UTENGENEZAJI WA SABUNI YA MCHE (MAGADI)

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI ZA MCHE (MAGADI)

UTANGULIZI

Sabuni ya magadi inatengenezwa kwa kutumia mafuta yenye sifa ya kuganda Kama vile mise ,mawese,na mafuta Nazi

Kwa nchi yetu ya Tanzania  mafuta yanayotumika sana  mise na mawese  kutokana na mafuta ya Nazi kuwa ghali

Ila mafuta ya mawese wengi huwa yanawasumbua Sana kwani yaanatakiwa kutolewa rangi na kuanza kutumika.

Mafuta ya mawese yanawahi Sana kuganda wakati wa kutengeneza. Tunatumia mafuta ya mise au mbosa kwa sababu mazuri yanatoa Sabuni mzuri zenye povu

Mikoa ambayo yanapatikana mafuta ya.mise kwa urahisi kigoma,mbeya,morogoro(ifakara), Tanga (magoloto)


MAHITAJI

1.MAFUTA YA MISE LITA 20

2.CAUSTIC SODA KG 3 NA GRAM 400

3.MAJI LITA 10.

4.SODIUM SILICATE ROBO LITA 

5.RANGI GRAM 25 AU vijiko viwili

6.hydrometer Kama unayo 

7.Mti wa kukorogea 

8.mask 

9.gloves kubwa ngumu

10.miwani

11.Mzani 



NOTE: JITAHIDI KUWA NA VIFAA KINGA KWA AJILI YA USALAMA WAKO

NOTE:  SABUNI ZA MAGADI AU MCHE ZINATENGENEZWA KWA SIKU TATU AU ZAIDI 


SIKU YA KWANZA

1.VAA GLOVES chukua chombo Cha plastiki weka maji Kisha weka caustic soda kidogo kidogo huku ukiwa unakoroga  koroga Kisha iache kwa masaa 24  ipoe 


NOTE: HAPA  KAMA UNATENGENEZA KWA MAFUTA LITA 20 HAPO. JUU UTACHANGANYA MAJI LITA  KUMI  NA CAUSTIC SODA KILO 3 NA 400 GRAM

 SIKU YA PILI 

2.Pima kwa hydrometer uweze kupata baume 30 Kama hauta pata baume 30 ikizidi utaongezea maji utakoroga ikipungua utaongezea caustic soda utakoroga Kisha utaona tena   Kama hauna usijali  ukishapima  weka sodium' SILICATE kwenye caustic solution Kisha koroga 

NOTE: Kumbuka caustic soda + maji = caustic solution.

3.chukua Jaba lako weka mafuta ukisha maliza Anza KUMIMINA caustic soda solution yako kidogo kidogo huku ukiendelea kukoroga mpka pale mchanganyiko wako utapoona umechanganyika vizuri  chukua ndoo ndogo chota mchanganyiko wako kiasi weka rangi Kisha koroga  ukimaliza

4.Andaa mold yako Kisha Anza KUMIMINA mchanganyiko ule mweupe Kisha fuata wenye rangi ya blue fanya hivyo Kama ilivyo kwenye video hizo hapo ukimaliza acha ukauke inategemea unaweza kukaa masaa 4 Hadi 6 au 12 inategemea Ila uwe unakuja kuangalia Kama imekauka

SIKU TATU 

5.Ikikauka TOA kwenye mold kisha Anza kukata  sabuni zako. Ziache zikauke. Tayari kwa KUPELEKA sokoni 


MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA KUKATA

kukata Ni rahisi Sana kama.utafuata vigezo hivi 

1.Uwe na mold mzuri  isiyo na mikunjo pemben

2.uwe mshipi (Uzi ) au copper wire

3.uwe na vibao visivyopungua kumi AMBAVYO vinafanana urefu ,upana na kimo na mche ambao umepanga utokeee

NOTE: KUMBUKA MAFUTA YA MISE NA MAWESE  YANATOKANA NA MTI MMOJA MCHIKICHI . MAWESE GANDA LA NJE na MISE  GANDA LA NDANI


Comments

Popular posts from this blog

FAIDA KATIKA BIASHARA YA MAHINDI TANZANIA

HATUA ZA KUFUATA, KILIMO BORA CHA UFUTA TANZANIA.

KILIMO BORA CHA MAHARAGE, TANZANIA